Breaking News

KUTOKA KINONDONI, MHE HAPI KATUMBUA WALIMU WAKUU 68 WA SHULE ZA MSINGI, 22 SEKONDARI BAADA YA KUBAINI KUWEPO WANAFUNZI HEWA

Mkuu wa wilaya ya kinondoni mhe ALLY SALUMU HAPI

Na Frank Wandiba

Katika kutekeleza ahadi ya serikali ya awamu tano ya kutoa elimu bure kuanzia darasa la awali  mpaka sekondari, wilaya ya kinondoni ilimefanya  uchunguzi  na kubaini  udanganyifu mkubwa  uliofanywa na wakuu wa shule 68 za msingi na 22 za sekondari.

 

Amekizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam, Mkuu wa wilaya ya kinondoni mhe ALLY SALUMU HAPI  alisema aliagiza kufanyika kwa uchunguzi hili kutekeleza agizo la mhe Rais MAGUFULI alilotoa kwa wakuu wa wilaya kuwachukulia hatua kali walimu wakuu  na watendaji wote  ambao watafanya udanganyifu na ubadhilfu  wa fedha  za elimu  bure.

 

Alisema kufatia agizo hilo aliagiza kufanyika uhakiki wa wanafunzi  darasa kwa darasa na tumebaini udanganyifu mkubwa, ambapo jumla ya wanafunzi  3,462 wa shule ya  msingi na 2,534 sekondari wamebainika kuwa ni hewa na fedha zao azikupaswa kupelekwa.

 

Baada kugundua udanganyifu huo ofisi yake tayali nimemwagiza  mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni awavue madaraka walimu wakuu 68 wa shule za msingi na 22 wa sekondari.

 

Aidha mhe HAPI alitoa rai kwa watendaji wengine wa wilaya ya kinondoni wasio waaminifu na wasiofuata sheria na taratibu kuwa popote walipo atawasaka na wasipo jirekebisha na kuendana sanjali na kasi ya mhe Rais.

 

Mwishoni mwa mwezi julai Raisi wa Jamhuri ya muungano  wa Tanzania Dr john magufuli alitoa maagizo  kwa wakuu wa wilaya  na wakurugenzi wote nchini kufuatilia kwa makini fedha za elimu bure hili kubaini udanganyifu na wizi unaofanywa na watendaji wasio waadilifu.

 

No comments