CCM DAR YATOA TAMKO ZITO MSAMAHA WA SPIKA NDUGAI
Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salam, kimesema hatua ya Spika wa Bunge, mheshimiwa Job Ndugai imeonyesha ukomavu wake kisiasa na kujutia hivyo inapaswa kusamehewa.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salam, Bi. Kate Kamba alisema bada ya Spika Ndugai kuomba radhi hakuna sababu ya kuendeleza marumbano juu ya suala hilo.
“Hatuna sababu ya kuendelea na marumbano ambayo yatazidi kutugawa. Umoja wa taifa letu ni mshikamano. Mshikamani ni wamaana sana kuliko haya mambo mengine,”alieleza Kate.
Alibainisha, mtikisiko wa sakata la Spika Ndugai badala ya kuwagawa watanzania lakini uliwaweka pamoja zaidi.
“Mtikisiko huu umechangia kuimarisha umoja wetu. Umeona watanzania jinsi walivyo kuwa wa moja. Tunampongeza ameomba radhi kwa watanzania walio kwazika. Imeonyesha ukomavu wake kisiasa,”alisema.
Alisema matukio mengi mengi yaliyotokea yamekuwa yakiwaweka watanzania pamoja na kwamba sakata la Ndugai lilikuwa fundisho.
“Tanzania tunao uhuru wa kuongea na kusahihishana. Ndugai alizungumzza maoni yake na ilionekana anaipenda Tanzania. Sisi ni wanadamu, tunapokoseana hata Mwenyezi Mungu usamehe,” alibainisha Kate.
No comments